Header Ads

NI RUKSA KUKATA TAMAA KATIKA MAENEO HAYA MAWILI

Habari  za siku mpenzi msomaji wa mtandao huu wa MTEGACHEM-IT. Ni matumaini yetu kwamba unaendelea vyema kabisa licha ya changamoto na majukumu mbalimbali  tunayokumbana  nayo kila kukicha, pole sana rafiki na usichoke kupambana. Mara baada ya kusema hayo tugeukie kwenye makala yetu ya leo. Kama ujuavyo kwamba ni kawaida ya mtandao huu kuwa na utaratibu maalumu wa kushirikisha wasomaji wake mambo mbalimbali ya kujifunza na kuhamasika. Hilo ndio lengo kuu la mtandao huu yaani kuwashirikisha ndugu zetu kile tunachojifunza na kukipitia. Kwani siri ya maisha ni kutoa. Kutoa ndio dhumuni la kila maisha ya mmoja wetu katika dunia hii. Na sisi kwa kulitambua hilo ndio maana kila siku tunakuja na kitu kizuri na kipya cha wewe kujifunza. Kwa hiyo, tunapenda na wewe uungane nasi katika safari hii ya utoaji kwa kutusaidia kuwafikia wengi zaidi ili waweze kutembelea mtandao huu kwa kuwashirikisha baadhi ya makala zetu iwe kwenye mitandao au ndani ya jamii yako ili nao waweze kujipatia mambo haya mazuri unayoyapata. Tutashukuru sana ikiwa utachukua hatua mara moja sasa katika kuwashirikisha na wenzako. Na kama nilivyokwambia awali kutoa ndio siri ya maisha na wale wanaotoa iwe misaada, mawazo yao n.k wataongezewa zaidi kulingana na kile wanachokitoa. Yaani tunavuna kile tunachokipanda. Naona nisiende mbali zaidi katika kukizungumzia kitu ambacho sio mada yetu kuu ya leo. Mada yetu ya leo sio kuhusiana na utoaji ila nitakuja kulizungumzia hili hapo mbeleni.

Katika makala yetu ya leo nakwenda kuzungumzia kuhusiana na suala la kukubali kushindwa  katika kile unachokifanya au upi ni wakati sahihi wa wewe kuacha kufanya jambo ulilokuwa ukilifanya. Naona mpaka hapo utakuwa unashangaa kwa nini nazungumzia ukubali kushindwa wakati kwa miaka kadhaa sasa nimekuwa nikihubiri na kuwahimiza wengi kutokukata tamaa. Ni haki yako kushangaa ila litakuwa ni jambo la muhimu zaidi ukaendelea kusoma makala hii mpaka mwisho ili uweze kung’amua ni nini hasa ninachotaka kukueleza na kumaanisha. Na ni matumaini yangu mara baada ya wewe kumaliza kusoma makala hii utakuwa umenielewa kwa kiasi fulani na utakuwa umefanikiwa kupata kitu cha kwenda kukifanyia kazi. Karibu katika mada yetu ya leo..

Kama tujuavyo kwamba siri mojawapo inayochangia mafanikio ya watu wengi zaidi  duniani  ni ile hali ya kutokukata tamaa, yaani kutokubali kushindwa katika kila jambo wanalolifanya au wapambane mpaka dakika ya mwisho ili wafanikiwe kupata kile wanachokitaka katika maisha yao. Nami kwa kulitambua hilo, kwa zaidi ya miaka miwili sasa nimekuwa nikiwasihi wasomaji wangu na wewe ukiwa mmoja wapo kamwe wasikubali kukata tamaa mpaka tone la mwisho ili tuweze kuona ndoto zetu zikitimia, yaani tupambane mpaka mwisho.

Sasa Geofrey, ikiwa umekuwa hukitusii kutokukata tamaa iweje leo uje na mada ya kukubali kushindwa? Una haki ya kuniuliza hivyo ili naomba unisikilize kwa makini..

Watu wengi sana katika  jamii zetu kwa zaidi ya miongo kadhaa sasa wamekuwa  wakihimizwa kutokukata tamaa au kutokuacha kufanya jambo mpaka wafanikiwe,  kwa maana nyepesi tunaweza kusema kwamba wameambia wasikubali kushindwa. hivi unajua sababu ya uwepo wa hali hiyo? Sababu ni kwamba; jamii yetu imekuwa ikiwachukulia watu wanaokata tamaa kama watu ambao hawatokwenda kufanikisha jambo lolote lile katika maisha. yaani watu hao hawatoweza kufanikiwa kabisa katika maisha iwe kwenye jambo dogo au kubwa. ila kwa upande wangu nadhani huu ndio wakati sahihi wa jamii zetu  kuanza  kufunguka na kuachana na imani potofu, yaani imani zisizokuwa na manufaa yoyote kwetu. Kwani wakati mwingine inatubidi tukubali tu kushindwa hasa wakati tunapokuwa tukitafuta kitu tunachopenda kukifanya (passion), na wakati tunapokuwa kwenye mazingira hasi. Na kuna nukuu maarufu imekuwa ikitumiwa sana na wengi japokuwa wengi wanaoitumia wamekuwa wakiipuuza ila ina maana kubwa sana ndani yake. Nukuu hiyo si nyingine bali ni kwamba” asiyekubali kushindwa si mshindani”. Hiyo ni nukuu nzuri na yenye maana kubwa ndani yake ikiwa utaielewa kwa upana zaidi.

Wakati sahihi wa kukata tamaa.
Hapo kabla nimekwambia kwamba wakati sahihi wa wewe kukata tamaa ni wakati unapokuwa unatafuta kile unachopenda kukifanya (passion) na wakati unapokuwa kwenye mazingira hasi. Na yafuatayo ni maelezo machache ya kwa nini ni ruksa kukata tamaa kwenye maeneo hayo mawili.

1.Unapokuwa unatafuta kile unachopenda kukifanya; kwa kweli ni ruksa tu kwako kukata tamaa wakati unapokuwa unatafuta kile unachopenda kukifanya. Sasa swali muhimu linalokuja hapa ni je wakati upi ukubali kukata tamaa? Ni pale unapokuwa haufanyi kitu unachokipenda au ukuwahi kukipenda kukifanya hapo kabla. kufanya kitu usichokipenda ni sawa na kupoteza muda wako bure, na ikiwa hauna furaha katika kile unachokifanya basi hakuna hitaji la kuendelea kufanya kitu hicho na ni muhimu ukaachana nacho kwani hautokuja kufanikiwa. Na kama utawaangalia kwa makini watu wote wenye mafanikio katika maisha utakuja kugundua kwamba watu hao wamefanikiwa kutokana na kufanya kile wanachokipenda na si vinginevyo. Kwa hiyo kuanzia sasa ni ruksa kukata tamaa unapofanya jambo usilolipenda.

2. Wakati unapokuwa kwenye mazingira hasi;  ishara ya pili ya wewe kukubali kukata tamaa ni pale unapokuwa  kwenye mazingira hasi. Yaani unapokuwa kwenye jamii yenye mitazamo hasi zidi yako. Kwani ni vigumu kwetu kukua na kuweza kufanikisha malengo pamoja na ndoto zetu ikiwa tutazungukwa na mazingira hasi. Na kama tujuavyo kwamba mara nyingi huwa tunatokana na wastani wa watu watano tunaotumia muda mwingi  tukiwa pamoja nao, na watu hao wanaweza wakawa ni rafiki zetu, ndugu n.k. Kwa hiyo hapa simaanishi  usishirikiane kabisa na watu hao bali ninacho maanisha hapa ni wewe kuchagua marafiki  vizuri,, na kama watakuwa ni  ndugu zako na ikiwa wana mitazamo hasi basi unatakiwa upunguze muda mwingi unaotumia kuwa pamoja nao. Ikiwa utakuwa kwenye mazingira ambayo kila mtu aliyepo humo ana mtazamo hasi basi ni ruksa kwako kukata tamaa kwa kuondoka mahali hapo na kuamua kwenda kwengine. Ni ruksa kukata tamaa kwenye maeneo hayo

No comments

Contact us:Email:godfreymtega@gmail.com/WhatsApp-+255758297744/+255716824009 . Powered by Blogger.