Header Ads

KRC Genk imelazimishwa sare na Lokomotiva ugenini, Samatta akipachika goli

Usiku wa August 18 2016 michezo ya Play offs ya kuwania kufuzu hatua ya makundi ya michuano ya UEFA Europa League ilichezwa katika viwanja mbalimbali barani Ulaya, moja kati ya michezo ya Europa iliyochezwa usiku wa August 18 ni mchezo kati yaLokomotiva Zagreb ya Croatia dhidi ya KRC Genk inayochezewa na Mbwana Samatta.
Katika mchezo huo uliyochezwa Croatia yaani katika uwanja wa nyumbani waLokomotiva, umemalizika kwa sare ya goli 2-2, Genk inayochezewa na mtanzaniaMbwana Samatta ilianza kupata goli la kwanza kwa mkwaju wa penati kupitia mjamaicaLeon Bailey dakika ya 47 na baadae Mbwana Samatta dakika ya 52.
photonews-10599199-101-jpg_1471547491
Licha ya kuwa Lokomotiva walikuwa nyumbani na kufanikiwa kusawazisha goli zote mbili kupitia kwa Mirko Maric dakika ya 51 na Ivan Fiolic dakika ya 59, KRC Genk ilitawala mpira kwa asilimia 60 na kuwaacha wenyeji wao wakimiliki mpira kwa asilimia 40, Kwa matokeo hayo Genk itahitaji suluhu au sare ya goli 1-1 katika mchezo wa marudiano August 25 katika uwanja wao nyumbani.

No comments

Contact us:Email:godfreymtega@gmail.com/WhatsApp-+255758297744/+255716824009 . Powered by Blogger.