Header Ads

Walichokusudia kufanya wanachama wa Yanga kesho August 16 kuhusu Yusuph Manji

Baada  ya taarifa za mfanyabiashara na mwenyekiti wa klabu ya Dar es Salaam Young Africans Yusuph Manji kuripotiwa kukusudia kujiuzulu wadhifa wake huo ndani ya klabu ya Yanga kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kuandamwa na maneno na baadhi ya watu huku wana Yanga wengine wakiwa kimya.
Taarifa za Manji kujitoa zinakuja kwa sababu ya kudaiwa kujihisi mpweke kwani licha ya kushambuliwa kwa maneno na baadhi ya ya watu ikiwemo wanasiasa, hakuna mwanayanga aliyekuwa pamoja nae hivyo anajihisi mpweke na ana kusudia kujiweka pembeni.
Kufuatia taarifa za Manji kukusudia kujitoa viognozi wa Yanga wa kanda zote wamekusudia kufanya kikao kesho saa 4 asubuhi makao makuu ya klabu hiyo kutoa tamko la pamoja kuhusianna maamuzi ya Manji, kujitoa kwa kuona anatengwa na wanachama.

No comments

Contact us:Email:godfreymtega@gmail.com/WhatsApp-+255758297744/+255716824009 . Powered by Blogger.