Header Ads

AYOTV VIDEO: Ziara ya kushtukiza aliyoifanya DC Ally Hapi katika hospitali ya Mwananyamala

August 18 2016 Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Dar es salaam Ally Hapi alifanya ziara katika hospitali ya Mwananyamala na kubaini mapungufu mbalimbali katika hospitali hiyo ikiwa ni pamoja na ubadhirifu wa fedha za wagonjwa ambapo inadaiwa hospitali hiyo imekuwa ikitozapesa ya kujiandikisha Shilingi elfu kumi badala ya elfu sita iliyoidhinishwa na Serikali.
DC Hapi amesema…>>>’Nimekuja kuangalia utozaji wa gharama za kadi kwa wagonjwa, nilipewa taarifa kwamba wagonjwa wamepandishiwa bei kutoka shilingi elfu sita hadi elfu kumi jambo ambalo linawafanya masikini kukosa huduma
Nilitoa maelekezo jana lakini bado wanaendelea kutoza elfu kumi, pia utaratibu wa kupandisha hizo fedha haukufuatwa na inaonekana inagusa hadi kwenye gharama za vipimo‘ –Ally Hapi
Nimeagiza fedha ishushwe ibaki vilie ilivyokuwa awali na pili Mkurugenzi na timu yake wachukue hatua kuhakikisha kila mmoja aliyehusika achukuliwe hatua stahiki akiwemo mganga mfawidhi wa hospitali ya Mwananyamala‘ –Ally Hapi


No comments

Contact us:Email:godfreymtega@gmail.com/WhatsApp-+255758297744/+255716824009 . Powered by Blogger.