Header Ads

ATHARI TATU(3) ZA KUJIKWEZA KUTOKANA NA MAFANIKIO ULIYOYAPATA

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa makala za mtandao huu(www.mtegachemit.blogspot.com) ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vyema katika kupambana ili tu kuweza kujiletea mafanikio, nami nakusihi endelea kupambana bila kuchoka maana mafanikio ni mapambano ambayo yanakuhitaji kuwa imara zaidi na zaidi. Karibu leo tujifunze kwa pamoja juu ya tabia moja ya kuiepuka pindi upatapo mafanikio.

Kila mtu kwa namna yake na kwa aina yake amekuwa akitafuta mafanikio na kuyapata, lakini sina uhakika kama katika wapambanaji hawa wanao pambana ili kuyapata mafanikio kuna anayetaka mafanikio ya muda mfupi kutokana na sababu hii ndio maana nakusihi sasa kuwa usijikweze kutokana na mafanikio uliyoyapata, maana wapo watu ambao pindi wapatapo mafanikio hujikweza na kujifanya kuwa wao ni mungu watu yaani wanajua kila kitu hawaambiliki, hawashauriki wala kufundishika kwa namna yoyote haswa na watu ambao wako chini yao kiuwezo. Zifuatazo ni athari za kujikweza na madhara yake

Kumbuka biblia inasema “ajikwezae atashushwa”, sio jambo la busara kwako wewe eti kisa una mafanikio basi ndio ukajiona bora sana kuliko watu wengine maana jambo hili linaweza kupelekea ukawa na dharau sana kwa watu wa chini yako na swala hili kama wewe ni mkuu/bosi wa kampuni fulani linaweza kuathiri sana utendaji wa kazi wa wafanyakazi wako na hatimae kampuni yako ikaja kufilisika maana hakuna mfanyakazi ambae anapenda kufanya kazi katika mazingira ambayo anadharaulika na dharau kwa wafanyakazi huwa inashusha morali yao ya kufanya kazi hivyo ni rahisi kwao wao kuanza kufanya kazi ovyo ovyo na hatimae kampuni ikakosa maendeleo kwa kiasi kikubwa.

Kujikweza hukufanya ushindwe kushaurika, kwa kuwa wewe unajikweza na kujiona kuwa wewe ndio wewe basi hata kama unashauriwa jambo zuri wewe utapuuzia maana unajiona wewe ndio wewe hivyo kusikiliza ushauri kwako inakuwa ngumu. Kutokusikiliza ushauri wa watu sio jambo la busara maana unaweza kupuuzia ushauri hata wenye tija, na kupuuzia huku hutokana na sababu kuwa wewe ushajikweza, yaani kama wewe ni bosi basi unaona kuwa mfanyakazi hawezi kutoa ushauri wowote wenye kunufaisha kampuni au shirika lako, jambo ambalo ni kupotoka maana kampuni bora na zinazofanya vizuri hapa duniani ni zile ambazo bosi anashirikiana vyema na wafanyakazi wake kwa kila jambo haswa bosi kusikiliza ushauri wa watu wa chini yake maana wao ndio wafanyakazi, kama ni bidhaa wao ndio watengenezaji, wao ndio wasambazaji na wauzaji hivyo wakikushauri kuhusu bei ya bidhaa mfano ni muhimu ukawasikiliza maana wewe upo kama msimamizi ambapo mambo mengi utakuwa huyajui kiuhalisia ila kupitia wao unaweza kuyajua.

Kujikweza kutakufanya usiwe msikilizaji bali uwe mzungumzaji tu, jambo jingine ambalo linaweza kuhatarisha mafanikio yako kutokana na kujikweza kwako ni kuwa , kutokana na kujikweza kwako basi wewe utabaki kuwa mzungumzaji kuliko msikilizaji jambo ambalo ni hatari sana katika maisha. Maishani watu wanaofanikiwa ni wale ambao wana uwezo mkubwa wa kusikiliza watu pindi wanapozungumza na sio wao wanataka kusikilizwa muda wote. Mtu anayependa kuzungumza muda wote kuliko kuwasikiliza wenzake anakuwa amejikweza na kujiona kuwa yeye ni bora kuliko sasa kama hupendi kuwasikiliza wenzako basi na wao ipo siku watachoka kukusikiliza vile vile na hapo ndipo utakapo pata anguko lako na kubaki kuyasikia mafanikio.

Nimekuwekea athari tatu muhimu ambazo zinaweza kukupata kutokana na kujikweza kwako hivyo hata kama una mafanikio kiasi gani hakikisha kuwa hujikwezi maana kujikweza huleta anguko na ukianguka katika mafanikio kuinuka huwa ni kazi ngumu sana.

No comments

Contact us:Email:godfreymtega@gmail.com/WhatsApp-+255758297744/+255716824009 . Powered by Blogger.