Header Ads

RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 34

Mtunzi:Enea Faidy

...Lakini cha ajabu kila alipomsogelea binti yule naye alikaza mwendo zaidi. Mama Dorice alishuhudia jinsi ambavyo mwanaye alitembea kwa madaha sana.

"Doriiiice!" Aliita kwa sauti lakini yule msichana alipogeuka hakuwa Dorice tena ilikuwa ni sura ya msichana mwingine kabisa. Mama Dorice alichanganyikiwa sana, ni kwanini hali inakuwa vile? Lakini hakupata jibu. Kaka yake alimfata haraka na kumshika mkono.
"Dada utagongwa na magari... Kwani unamfata nani?" Aliuliza kwa mshangao kwani yeye hakumwona MTU yeyote.
"Namfuata Dorice..."
"Huyo Dorice yuko wapi maana tangu tupo kule unamfuata tu?"

"Sio yeye.. Nimemfananisha...."
"Dada bwana usiwaze sana.... Ona sasa mpaka watu wanakushangaa ujue.. Unaita kila mtu Dorice..."
"Lakini Mimi nilimwona kabisa kaka...."
"Haya tuondoke"
Mama Dorice alikuwa bado anaifikiria ile hali, akajua lazima kuna kitu kinaebdelea kuhusu Dorice, kwanini amfananishe kiasi kile lakini bado hakuwa na jibu sahihi.

Wakati wa safari ulipowadia, waliingia kwenye basi na kukaa kwenye siti zao.Walisafiri kwa mwendo kidogo, ndipo macho ya mams Dorice yalipotua kwenye sura ya yule binti aliyemwona toka wakiwa kituo cha mabasi Jana yake. Na alikuwa amevaa nguo zile zile, alikaa Pembeni yake. Moyo ulimpasuka kwa mshtuko akafikinya macho yake na kumtazama tena binti yule aliyeachia tabasamu mwanana. Akamsalimu mama Dorice. Mama Dorice alishangaa, kilichomshangaza zaidi ni kwamba alipoingia kwenye gari hakumwona MTU yule na hata alipokaa hakukaa na binti yule. Sasa imekuaje yupo nae?
 
"Mama nilikuona sehemu!"
"Mh hata Mimi nilikuona!" Alisema mama Dorice.
"Kwanini ulikuwa unanifata?" Aliuliza binti yule ambaye kila wakati alipenda kutabasamu.
"Nilikuwa na kufananisha na mwanangu" alisema mama Dorice.

"Mwanao? Anaitwa Dorice?"
"Ndio... Umemjuaje?"aliuliza mama Dorice lakini msichana yule alicheka sana kitendo kilichomshangaza mama Dorice.
"Mama we si uliniita Dorice?"
"Eeh ndo jina lake.." Wakati wakiendelea na mazungumzo Yale mjomba wake Dorice alimshangaa sana dada yake.
"Dada mbona unaongea peke yako? Unajibizana na nani?"


==>Endelea  Nayo <<kwa Kubofya Hapa>>

Advertisement
==

No comments

Contact us:Email:godfreymtega@gmail.com/WhatsApp-+255758297744/+255716824009 . Powered by Blogger.